Saturday, 30 April 2016

Msimamo VPL Leo: Yanga Bado Points Hizi Hapa Kunyaka UBINGWA WA 26



Matokeo yote ya mechi za Jumamosi
Yanga imeendelea kushinda mechi zake za ligi kuu Tanzania bara baada ya kuifunga Toto Africans ya jijini Mwanza kwa magoli 2-1 kwenye uwanja wa CMM Kirumba, Mwanza.
Toto walianza kupata goli la kwenye mchezo huo lililofungwa na William Kimanzi dakika ya 39 kipindi cha kwanza lakini goli hilo likasawazishwa na Amis Tambwe dakika ya 50 kipindi cha pili.
Yanga walijihakikishia pointi tatu kwenye mchezo huo kupitia beki wao wa kulia Juma Abdul dakika ya 78 na kifanya Yanga kufikisha pointi 65 baada ya kucheza michezo 26 ya VPL.
Mwadui 2-1 Stand United
Prisons 1-1 JKT Ruvu
Mtibwa 1-0 Mbeya City
African Sports 1-0 Coastal Union
Toto Africans 1-2 Yanga

Kila ra heli Farid Musa





Cheki taswira, kinda wa Azam FC, Farid Mussa akiwa katika majaribio kuwania nafasi acheze soka la kulipwa barani Ulaya. Hapa Farid anafanya majaribio katika klabu ya Club Deportivo Tenerife Hispania. Leo ametimiza siku ya nne katika majaribio na taarifa zinasema anaendelea vizuri.

Awali, Farid alisema ana imani kubwa kwamba atapasi majaribio hayo kwa kuwa ndiyo kitu alichokuwa anakihitaji na atakipigania kwa nguvu zote.

Hata hivyo, Farid alikubali kwamba anaona Hispania wamepiga hatua kubwa kimaendeleo katika soka, jambo ambalo ni zuri kwake kwa kuwa atajifunza zaidi.

PICHA KWA HISANI YA AZAM FC.


JE ? Licester City kutangazia ushindi old trafod



Na Saleh Ally
IDADI kubwa ya wadau wa soka hapa nyumbani Tanzania, England na kwingineko duniani wanajiuliza swali moja tu muhimu. Kweli Manchester United itakubali kuwa ngazi, ipigwe na Leicester City iwe bingwa wa England kwa mara ya kwanza?
Kama Leicester ambayo iko ugenini kesho kwenye Uwanja wa Old Trafford itashinda dhidi ya Man United, basi itakuwa imefikisha pointi 79 tofauti ya pointi 10 dhidi ya Tottenham Hotspur ambao wanashika nafasi ya pili.
Kama ni hesabu, inaonekana hivi, ni lazima Leicester watakuwa mabingwa wa England msimu huu. Kama ni miujiza, basi ina uwezo wa kuwazuia kwa asilimia 10 pekee, kwa kuwa mpira nao hauaminiki.

Lakini kusema lazima watakuwa mabingwa, bado inawezekana kwa asilimia 90. Kwani hata kama kesho watapata sare dhidi ya Man United, bado wanaweza kutangazwa mabingwa rasmi keshokutwa Jumatatu kama Tottenham watapoteza mchezo wao dhidi ya Chelsea wakiwa ugenini Stamford Bridge.
Hata hivyo, bado mechi ya kesho ndiyo inabaki kuwa kila kitu kwa Leicester ambao kama watabeba ubingwa, basi ni wachezaji hadi kocha watakuwa wameweka rekodi na kufanya mabadiliko huku wakiweka kumbukumbu ya Blackburn Rovers iliyopanda daraja na kubeba ubingwa wa Ligi Kuu England msimu wa 1994-95.

Mechi zilizopita:
Manchester United haina nguvu ya kufukuzana na Leicester kama utazungumzia ubingwa lakini katika mechi zake sita zilizopita, imeshinda nne na kupoteza mbili. Leicester imeshinda tano na sare moja.
Kwa mwendo, Leicester wako vizuri zaidi lakini kamwe hauwezi kuwabeza Man United kwa kuwa mwishoni kikosi chao kinaonekana kuwa vizuri zaidi na wamefanikiwa kuingia fainali ya Kombe la FA.
Ugenini:
Leicester ni kati ya timu bora zinapokuwa zinacheza ugenini. Kwani kati ya michezo 12, imeshinda mechi 10, imetoka sare 1 na kupoteza 1. Hii inaipa asilimia 71 za ushindi inapokuwa nje ya nyumbani.
Hivyo katika pointi zake 67 katika msimamo sasa, 31 imefanikiwa kukusanya ikiwa ugenini. Hili si jambo dogo na Man United hawapaswi kuibeza Leicester hiyo kesho.

Kwa Manchester United, wakiwa nyumbani inaonekana hivi; katika mechi 11, wameshinda 11 bila sare au kupoteza. Maana yake wana asilimia kubwa zaidi ya kufanya vizuri nyumbani.
Mechi hii itakuwa burudani ya aina yake na huenda ikawa gumzo kwa kuingia kwenye historia ya soka la England.
Presha:
Katika mechi hiyo, wanachotaka Manchester United ni kupata nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya, yaani Top Four, japokuwa bado watakuwa hawataki kugeuzwa ngazi hiyo kesho na kuingia kwenye historia kuwa wa mwisho ‘kuisaidia’ Leicester kuwa bingwa.
Kwa Leiceter, lazima watakuwa kwenye presha kubwa kidogo ambayo inaweza kuwa msaada au tatizo kwao. Kuwa mabingwa ni jambo ambalo wana hamu kubwa, pia wana hofu kuu ya kufungwa. Haya wakiyachanganya vibaya, huenda yatawaangusha na wakashindwa kucheza mpira wao.

Mechi 5:
Katika mechi tano za mwisho ambazo Man United imecheza. Imefanikiwa kufunga mabao manne ikafungwa matatu wakati ilipopoteza kwa mabao 3-0 dhidi ya Tottenham. Man United inaonekana iko makini kwenye ulinzi, lakini ikiotewa, kweli inalainika.
Leicester, mechi zao tano wamezicheza hivi, wameshinda mabao tisa, wakaruhusu mabao manne. Aina ya uchezaji inaonekana ni ‘open game’. Mchezo ambao si wa ulinzi mwingi sana na wanaweza kukufunga mabao mengi ukizubaa lakini wanafungika.
Mara ya mwisho:
Mara ya mwisho zilikutana Novemba 28, mwaka jana ikiwa ni mechi ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu England. Matokeo yalikuwa 1-1 licha ya Man United iliyokuwa ugenini kwa bao la kusawazisha la kiungo Mjerumani Bastian Schweinsteiger.
Hii inaonyesha hata mechi ya kesho, haitakuwa rahisi kwa kila timu. Ingawa Leicester lazima wacheze wakitaka ushindi hata kama sare inaweza kuwapa ubingwa.
Wanakosekana:
Kila upande utakosa watu muhimu, wageni Leicester kama kawaida, mshambuliaji wao nyota Jamie Vardy anaendelea kutumikia adhabu ya kufungiwa. Walimkosa katika mechi iliyopita dhidi ya Swansea, lakini wakashinda 4-0 wakiongozwa na Riyad Mahrez.
Manchester nao wana kazi kidogo, wanaendelea kuwakosa wachezaji kama Schweinsteiger aliyewakomboa wakiwa ugenini dhidi ya Leicester. Pia Luke Shaw, Will Keane na Adnan Januzaj nao wanakosekana. Hawawezi kuwa athari kubwa kwa Man United kwa kuwa wamekuwa nje kwa mechi kadhaa na imeendelea kupambana.
Wabetishaji:
Kampuni nyingi za kubeti za England zinaonekana kutoa nafasi kubwa kwa Man United kushinda mechi hiyo, wakiamini presha kubwa itawamaliza Leicester.
 Inaonekana wanaocheza mchezo huo, wengi wamechanganyikiwa, lakini wahusika wakuu, wamewapa nafasi Man United kwamba wana nafasi kubwa kutokana na mwendo.

Ingawa wafanyabiashara wa ubetishaji, pia ni wajanja wanaweza kulalia wanakoona, kutaharibika ili kutengeneza biashara yao.

Azam wakijiandaaa kummaliza Mnyama







Tuesday, 26 April 2016

MASHABIKI WA ARSENAL KUANDAMA KUMPINGA BOSS

Arsenal fans hold banners by hassan

Mashabki wa timu ya Arsenal wanajiandaaa kuaandaaa maandamano makubwa kwa ajili ya kumpinga bossi wa timu hiyo Kronke kutokana na maendeleo mabovu ya timu yao hasa kitendo chake cha kutowekeza kwenye na kusababisha timu kukosa mataji makubwa kama EPL na champions legue  ,

Mashabiki hao wanaendelea kulalamika kuwa wanataka mabadiliko kuanzia kocha wao na maswara mazima ya usajiri kwa timu kuchukua wachezaji wenye uwezo mkubwa  ,

Maaandamano hayo yamepangwa kuanzia mechi ijayo na Norwich City na kuendelea na wamepangwa kutumia mabango mbalimbali na kampane hiyo itaitw "MUDA WA MABADILIKO"  Time fo change

kwa habari zaidi soma daily mirror
http://www.mirror.co.uk/sport/football/news/arsenal-supporters-groups-unite-biggest-7837135?ICID=FB_mirror_MF

Samata Aumia timu yake ikilala

Na hassan luambano
STRAIKA aliyeanza kuteka nyoyo za mashabiki wa KRC Genk ya Ubelgiji, mtanzania Mbwana Samatta leo alilazimika kutoka uwanjani katika dakika ya 45 kwenye mchezo wa ligi kuu nchini humo dhidi ya AA Gent baada ya kugongwa na kuumizwa vibaya  puani.

Samatta alikutana na dhoruba hiyo mara baada ya kuanza kwa kipindi cha pili ambapo aligongana na beki wa Gent na kupata maumivu makali yaliyompelekea kushindwa kuendelea na mchezo huku nafasi yake ikichukuliwa na Nikos Karelis.

Taarifa za awali zinasema Samatta amevunjika pua huku mwenyewe akiieleza kuwa ana maumivu makali sana na leo jumatatu ndipo atapata majibu ya vipimo yatakayoonyesha atalazimika kukaa nje kwa múuda gani.

"Nasikia maumivu makali sana, kwasasa sijajua kama kukaa nje itakuwa ni kwa muda gani, ila kesho (leo) ndio nitajua," alisema Samatta.

Wakati Samatta anatolewa nje, timu hizo zilikuwa sare ya bao 1-1 lakini bao la dakika ya 90 la Renato Neto wa Gent alilopachika wavuni kwa mkwaju wa penati, liliwalaza wenyeji Genk mapema na kupoteza pointi tatu.

Genk inabakia katika nafasi ya nne kwenye ligi hiyo iliyo kwenye hatua ya sita bora (Play Off I) ikiwa imejikusanyia pointi 33 huku vinara Club Brugge wakiwa na pointi 41

ANGALIA MNYAMA ANAVYOJIANDAAA KULAMBA ICREAM YA AZAM UKO UNGUJA

Simba wanajiandaa na mchezo wa ligi kuu dhidi ya Azam jumapili, hapa makipa wa timu hiyo Manyika Jr na Vicent Angban wakiwa mazoezini huko Zanzibar.

Simba imeshajikusanyia pointi 57 ikiizidi Azam kwa pointi mbili, mechi hiyo itatoa taswira ya nani kati ya Simba na Azam atakuwa mpinzani wa Yanga kwenye mbio za ubingwa.

Kama Simba itashinda itafufua upya matumaini yao ambayo yalififishwa na Toto Africans baada ya kufungwa bao 1-0 katika mchezo wao wa mwisho wa ligi

Kocha Jackson Mayanja anataka kuona kikosi hicho kinapata nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa mwakani na njia pekee iliyobaki kwao ni kubeba ubingwa wa Bara.

Kiungo Said Ndemla, mmoja kati ya nyota wa Simba waliokuzwa klabuni hapo.

Baada ya kutolewa kwenye michuano ya Shirikisho, Simba wamebaki na jukumu moja tu la kubeba ubingwa wa bara, je, kikosi hiki kitaweza kuibuka na ubingwa huo ili wapate nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa?



Manyika Jr akichupa kudaka mpira katika mazoezi yanayoendelea kisiwani Unguja.

SPURS CHALI Leicester city Ubingwa unanukia

MATUMAINI ya Tottenham Hotspur kutwaa Ubingwa wa England yamepata pigo kubwa hapo Jana Uwanjani kwao White Hart Lane Jijini London walipotoka Sare 1-1 na West Bromwich Albion kwenye Mechi ya BPL, Ligi Kuu England.
Spurs walitangulia kufunga kwa Bao la Dakika ya 33 baada Beki wa WBA Craig Dawson kujifunga mwenyewe lakini Beki huyo huyo akarekebisha mambo kwa kusawazisha Bao katika Dakika ya 73.
Katika Mechi hii, iliyoisha 1-1, mara 3 Spurs walipiga Posti.
Matokeo hayo yamewafanya Vinara wa BPL, Leicester City, kuhitaji Pointi 3 tu toka Mechi zao 3 zilizosalia ili kutwaa Ubingwa.
Hivi sasa Spurs wapo Pointi 7 nyuma ya Leicester na ili kubaki na matumaini ya Ubingwa lazima washinde Mechi zao 2 na Sare 1 katika Mechi zao 3 zilizobaki na kuomba Leicester wate
DONDOO MUHIMU:
-Leicester wanahitaji Pointi 3 katika Mechi 3 zilizobaki kutwaa Ubingwa na hii ikiwa Tottenham watashinda Mechi zao zote.

Hii inamaanisha Leicester wanaweza kutwaa Ubingwa kwa mara ya kwanza katika Historia yao Jumapili ijayo ikiwa wataifunga Manchester United huko Old Trafford.
MECHI za mwisho:
Leicester City
Tottenham Hotspur
Jumapili 1 MeiMan United (a)
Jumatatu 2 MeiChelsea (a)
Jumamosi 7 MeiEverton (h)
Jumapili 8 MeiSouthampton (h)
Jumapili 15 MeiChelsea (a)
Jumapili 15 MeiNewcastle (a)
MSIMAMO:
LIGI KUU ENGLAND      

PATA VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI YETU LEO

Monday, 25 April 2016

WAJUE WAKALI WA YANGA SHILIKISHO CAF


Esparenca
Na Hassan Luambano

Grupo Desportivo Sagrada  Esperanca  kutoka Angola wamefikia tena rekodi yao kwenye michuano ya ngazi ya vilabu barani Afrika. Mara ya mwisho kuweka rekodi yao ya juu kwenye michuano hii ilikua mwaka 2005 pale walipotolewa na Asec Abidjan ya Ivory Coast kwa jumla ya magoli 3-2 raundi ya 16 bora klabu bingwa barani Afrika.
Mwaka huu watacheza na Yanga ya Tanzania kwenye raundi ileile ya 16 bora lakini siyo klabu bingwa Afrika bali ni kombe la shirikisho. Esperanca wamefanikiwa kukutana na Yanga baada ya kutolewa na Vita Klabu ya Jamuhuri ya  Kongo ambapo  Yanga walitupwa nje na Al Alhy ya Misri kwenye mashindano ya klabu bingwa Afrika.
Kuelekea mchezo wa kwanza kati yao ambao utachezwa kati ya Mei 6 hadi 8 jijini Dar es Salaam kabla ya marudiano huko Angola wiki mbili baadaye makala hii inakupa mambo muhimu kuhusu klabu hii ya Angola.
Historia Fupi Ya Esperanca
Esperanca ilianzishwa 22/12/1976 mjini Dundo, kwenye jimbo la Lunda Norte Nchini Angola. Jimbo hili ambalo Esperanca wanatoka kwa Kaskazini Mashariki limepakana na Jamuhuri ya Kongo, lina sifa ya kuwa na madini mengi ya dhahabu na almasi, hivyo Esperanca kwa Tanzania unaweza kuifananisha na Mwadui FC ya Shinyanga inayomilikiwa na mgodi wa almasi.
Segrada Esperanca ni neno la kireno lenye maana ya ‘Matumaini Takatifu’ (sacred hope), hivyo kutokana na wamiliki wa klabu hii, kampuni ya madini ya Diamond Company Diaming ambayo kwa sasa kampuni hii inaitwa Endima kulipenda shairi la aliyekuwa rais wa Angola kipindi hicho Agustino Neto, shairi ambalo lilitwa Segrada Esperance wakaamua kuipa timu yao jina la shairi hilo.
Uwanja wao wa nyumbani ni Estadio Segrada Esperanca wenye uwezo wa kubeba jumla ya watazamaji 3000.
Mafanikio ndani ya Angola
Esperanca ndani ya Angola wamefanikiwa kunyakua vikombe vitatu hadi sasa. Ligi ya Angola iitwayo Girabola  wametwaa mara moja mwaka 2005 wakati kombe la FA wamechukua mara mbili mwaka 1988 na 1999.
Mashindano ya CAF
Esperanca hawana mafanikio makubwa sana kwenye michuano ya Caf, mwaka 2005 walifika hatua ya 16 bora mashindano ya klabu bingwa Afrika, pia waliishia hatua za awali za kombe hili mwaka 2006.
Mwaka 1992, 1998 walishiriki mashindano ya kombe la shirikisho ambapo waliishia raundi ya pili, mwaka 1992 na mwaka 1998 waliishia raundi ya kwanza.
Pia Esperanca waliishia raundi ya pili mwaka 1989 na 2000 kwenye  kombe la washindi barani Afrika ambalo kwa sasa halipo tena.
Wachezaji wa nje
Kwenye kikosi cha sasa timu hii ina wachezaji wakigeni watano. Wachezaji hao ni golikipa Johhy mwenye miaka 34 kutoka Jamuhuri ya Kidemoklasia ya Kongo, mlinzi wa kulia Zibakaka kutoka Kongo umri miaka 22, pia kuna mlinzi mwingine kutoka Ghana anaitwa Seth umri miaka 26 pamoja na wachezaji wawili kutoka Ureno kiungo Oliveira miaka 32 na mshambuliaji Ary mwenye miaka 27.

  • Esperanca kwa sasa wanafundishwa na kocha kutoka Serbia, Zoran
  • Timu hii inatoka mji wa Dundo, mji wenye utajiri wa madini ya dhahabu na almasi.
  • Mackic.
  • Wana wachezaji watano raia wa kigeni, wareno wawili, wakongo wawili na mghana mmoja.

JUVE YATWAAAA UBINGWA NA KUWEKA HISTORIA


Juventus imeshinda taji la Serie A kwa mara ya tano mfululizo!
Ushindi wa bao 1-0 ilioupata Roma dhidi ya Napoli leo umeipa ubingwa wa Scudetto timu ya Juventus.
Juventus ilanza vibaya msimu wa 2015-26 baada ya msimu uliopita kunyakua mataji mawili na kufika hatua ya fainali ya Champions League na kupoteza mbele ya Barcelona.
Wakiwa bila ya nyota wao Andrea Pirlo na Carlos Tevez haikuwa rahisi kwao kufanya vizuri na hilo lilithibitika mwanzoni mwa msimu kabla ya kukaa sawa.
Kikosi hicho kilicho chini ya Massimo Allegri kilizinduka na kuanza kuikimbiza Napoli iliyokuwa kwenye kiwango bora mwanzoni mwa msimu, Juve waliipiga bao Napoli wiki chache zilizopita na kufanikiwa kutetea ubingwa wao.
Juve-bingwa 1
Ukiangalia namna Juventus walivyoanza ligi, inashangaza kuona wametangaza ubingwa kukiwa bado kuna mechi kadhaa mbele.
Uwepo wa Gianluigi Buffon, Paul Pogba pamoja na ukuta imaara lakini wakati huo wakiwa na Juan Cuadrado, Paulo Dybala na Alvaro Morata ilikuwa ni sababu tosha ya wao kutwaa taji la Serie A
Taji hilo ni la tano mfululizo kwao kwenye ligi ya Serie A lakini wengi wanatamani kama Juventus ingefanikiwa kupenya mbele ya Bayern Munich kwenye michuano ya Champions League na kusonga mbele.
Video ya wachezaji wa Juventus wakishangilia ubingwa wao wa tano mfululizo kwenye Serie A