Saturday, 23 April 2016

BILA RONALDO, REAL WATOKA NYUMA NA BALE KUIPA USHINDI

BALE-USHINDIWAKICHEZA Ugenini bila ya Nyota wao Cristiano Ronaldo ambae ni Majeruhi, Real Madrid walitoka nyuma kwa Bao 2-0 na kuifunga Rayo Vallecano 3-2 kwenye Mechi ya La Liga.
Rayo waliongoza 2-0 ndani ya Dakika 14 kwa Bao Adrián Embarba na Ladislao “Miku” Fedor lakini Real wakajikongoja na kufunga Bao la kwanza kupitia Gareth Bale na kusawazisha kupitia Lucas Vázquez alieingizwa kumbadili Karim Benzema alieumia.
Bale ndie alieipa Real ushindi kwa kufunga Bao la 3 zikibakika Dakika 9 Mpira kwisha.
MAGOLI:
Rayo Vallecano 2
-Adrian Embarba 7
-Nicolas Fedor Miku 14
 Real Madrid 3
-Gareth Bale 35
-Vazquez Lucas 52
-Gareth Bale 81
Ushindi huu umewaweka Real wakiwa kileleni mwa La Liga Pointi 2 mbele ya Barcelona na Atletico Madrid ambbazo zitacheza Mechi zao za mkononi baadae Usiku huu.

Magazetini Leo Jumapili 24, April 2016



20160424_043444
20160424_043456
20160424_043512
20160424_043521
20160424_043552
20160424_043605
20160424_043616
20160424_043636
20160424_04362520160424_043646
20160424_043658
20160424_043710
20160424_043724
20160424_043732
20160424_043743
20160424_043753
20160424_043804
20160424_043813
20160424_043825
20160424_043834

MWAMBA MAMADOU SAKHO ACHUNGUZWA NA UEFA

 
Mchezaji wa eneo la ulinzi wa Liverpool mwamba Mamadou Sakho anachunguzwa na shirikisho la mchezo wa soka barani ulaya(UEFA)baada ya kufeli vipimo vya madawa ya kuongeza nguvu michezoni.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 26,bado hajasimamishwa rasmi,hatajumuishwa kwenye kikosi cha Liverpool wakati uchunguzi wake ukiendelea,klabu ya Liverpool ilisema.
Sakho alinunuliwa kutoka PSG kwa ada ya pauni milioni 18 mwaka 2013,ameichezea Liverpool michezo 34 katika mashindano yote,timu yake inashika nafasi ya saba kwenye msimamo wa ligi kuu ya England inategemewa kuialika Newcastle United kwenye uwanja wa Anfield Jumamosi ya leo.

ZIFAHAMU TIMU ZITAKAZOCHEZA MICHUANO YA ULAYA KATIKA LIGI YA UINGELEZA EPL

BPL-UCL-EUROPAWASHABIKI wa Soka wa England wamegubikwa na kutojua ni Timu ngapi na za nafasi gani kwenye Ligi Kuu England zitashirikishwa kucheza UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI na EUROPA LIGI kwa Msimu ujao.BPL-APR22
IFUATAYO ni Taarifa inayofafanua hali halisi:
-BPL, LIGI KUU ENGLAND na Nafasi zake kucheza Klabu Ulaya:
England ina Nafasi 4 [Inaweza zikawa 5] kwenye UCL na 3 kwenye EUROPA LIGI.
Bingwa wa BPL ataingia moja kwa moja Hatua ya Makundi ya UCL pamoja na Mshindi wa Pili na wa Tatu.
Atakaemaliza Nafasi ya 4 ataanzia Raundi ya Mwisho ya Mchujo ya UCL ambayo husaka Timu za kuingia Hatua ya Makundi.
Bingwa wa FA CUP atacheza Hatua ya Makundi ya EUROPA LIGI na Bingwa wa Kombe la Ligi, Capital One Cup, atacheza Raundi ya Mwisho ya Mchujo ya EUROPA LIGI.
Ikiwa Bingwa wa sasa wa Kombe la Ligi, Man City, watafuzu kucheza UCL Msimu ujao basi Nafasi yake ya kucheza EUROPA LIGI itakwenda kwa Timu moja itayomaliza Nafasi ya juu kwenye Msimamo wa BPL [Fuatilia ufafanuzi zaidi chini].
-Uwezekano wa Timu 5 za BPL kucheza UCL:
Hili litawezekana ikiwa Liverpool watabeba EUROPA LIGI na pia kumaliza nje ya 4 Bora ya BPL.
-Uwezekano wa Timu ya 4 ya BPL kutocheza UCL:
Ikiwa Manchester City watabeba Ubingwa wa UCL na kumaliza Nafasi ya 4 kwenye BPL basi wao watatetea Ubingwa wao wa UCL kuanzia Hatua ya Makundi na hakuna Timu nyingine itayochukua Nafasi yake ya 4 ya BPL kucheza UCL.
Ikiwa City watatwaa UCL na kumaliza nje ya 4 Bora za UCL basi ile Timu ya 4 ya BPL itapelekwa kucheza EUROPA LIGI.
-Nafasi 3 za kucheza EUROPA LIGI:
Kucheza EUROPA LIGI katika Hatua za Makundi hufuatia Nafasi Timu iliyomaliza kwenye BPL kama inavyoelezwa chini, au kutwaa FA CUP huku Bingwa wa Capital One Cup huanzia Raundi ya 3 ya Mchujo ya EUROPA LIGI.
Kwa kutwaa Capital One Cup Mwaka 2016, Man City watacheza Raundi ya 3 ya Mchujo ya EUROPA LIGI.
Ikiwa City watafuzu kucheza UCL kutokana na kumaliza ndani ya 4 Bora ya BPL au kutwaa Kombe la UCL, basi nafasi yao kucheza EUROPA LIGI itatwaliwa na Timu nyingine ya BPL kama inavyoelezwa chini:
-Kumaliza Nafasi ya 4 kwenye BPL kutawezesha Timu kucheza EUROPA LIGI ikiwa…
Manchester City watatwaa UCL na kumaliza nje ya 4 Bora ya BPL [Labda Liverpool wamalize Nafasi ya 4 ya BPL na pia kutwaa EUROPA LIGI].
-Kumaliza Nafasi ya 5 kwenye BPL kutawezesha Timu kucheza EUROPA LIGI ikiwa…
Manchester City hawatatwaa UCL.
-Kumaliza Nafasi ya 6 kwenye BPL kutawezesha Timu kucheza EUROPA LIGI ikiwa…
Manchester City wakimaliza ndani ya 4 Bora.
-Kumaliza Nafasi ya 7 kwenye BPL kutawezesha Timu kucheza EUROPA LIGI ikiwa…
Manchester United wakitwaa FA CUP na kumaliza ndani ya Timu 6 Bora na Man City wakiwemo ndani ya 5 Bora.
-Kumaliza Nafasi ya 8 kwenye BPL kutawezesha Timu kucheza EUROPA LIGI ikiwa…
Liverpool watatwaa EUROPA LIGI na kumaliza Nafasi ya 7 ya BPL na Man United kutwaa FA CUP na kumaliza ndani ya 6 Bora za BPL na pia Man City wakifuzu kucheza UCL ama kwa kumaliza ndani ya 4 Bora za BPL au kutwaa UCL.
-Klabu ambazo hazitaweza kucheza EUROPA LIGI…
Timu itakayofungwa Fainali ya FA Cup.

PATA VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI YA LEO

20160423_051923
20160423_051936
20160423_052012
20160423_052026
20160423_052045
20160423_052055
20160423_052107
20160423_052118
20160423_052135
20160423_052145
20160423_052156
20160423_052207
20160423_052218
20160423_052231
20160423_052243
20160423_052253
20160423_052306
20160423_052315
20160423_052325
20160423_052334
20160423_052346
20160423_052355
20160423_052406
20160423_052421
20160423_052435
20160423_052445
20160423_052457
20160423_052508