Mfanyabiashara maarufu wa kiarabu
Dk Sulaiman Al-Fahim ametangazwa
kuwa mwenyekiti mtendaji wa klabu ya African Lyon
ambayo itashiriki ligi
kuu ya Tanzania Bara msimu ujao.
Mmiliki wa klabu ya African Lyon, Rahim Kangezi alisema kuwa waliamua kumuomba
Mmiliki wa klabu ya African Lyon, Rahim Kangezi alisema kuwa waliamua kumuomba
Al Fahim kushika nafasi hiyo kutokana na uzoefu wake katika
michezo hasa mpira wa
miguu mbali ya kuwa mfanyabiashara bilionea katika
nchi za Uarabuni na duniani kwa ujumla.
Kangezi alisema kuwa Al Fahim ni Rais wa kampuni ya Arab Union for Real Estate
Kangezi alisema kuwa Al Fahim ni Rais wa kampuni ya Arab Union for Real Estate
Development ya Dubai na miaka ya nyuma alikuwa
msemaji wa
kampuni inayomiliki klabu tajiri duniani, Manchester City,
Abu Dhabi
United Group (ADUG). ADUG iliinunua Manchester City Septemba, 2008.
Pia Al Fahim alitaka kununua klabu ya Portsmouth ambayo ilikuwa inashiriki
Pia Al Fahim alitaka kununua klabu ya Portsmouth ambayo ilikuwa inashiriki
ligi kuu ya Uingereza, lakini mpango huo haukuweza
kukamilika.
Kangezi alisema kuwa Al Fahim ataanza kazi rasmi Aprili 16 ambapo atatangaza timu yake ambayo
Kangezi alisema kuwa Al Fahim ataanza kazi rasmi Aprili 16 ambapo atatangaza timu yake ambayo
atafanya nayo kazi katika kuibadili klabu
hiyo na kuwa klabu bora Tanzania na bara la Afrika.
Alisema kuwa uwepo wa Al Fahim kutaifanya timu hiyo kuwa na
Alisema kuwa uwepo wa Al Fahim kutaifanya timu hiyo kuwa na
uongozi
bora wenye kujua uendeshaji wa
kisasa katika masuala ya mpira kwa
kuzingatia uzoefu wa mfanya biashara huyo mzoefu katika soka na michezo
mengine.
“Haikuwa kazi rahisi Al Fahim kukubali kuingia kwenye uongozi wa klabu yetu, ila tunashukuru
“Haikuwa kazi rahisi Al Fahim kukubali kuingia kwenye uongozi wa klabu yetu, ila tunashukuru
kwani alituelewa baada ya kukutana naye
alipokuja hapa nchini kwa shughuli zake”, alisema Kangezi.
Alisema kuwa lengo lake ni kuona African Lyon inakuwa klabu ya mfano si tu kwa Tanzania
Alisema kuwa lengo lake ni kuona African Lyon inakuwa klabu ya mfano si tu kwa Tanzania
, hata kwa nchi za Afrika Mashariki na Afrika kwa
ujumla. Kangezi alisema kuwa mipango yao ya
awali ni kuimarisha timu ya
kwanza ili iweze kufanya vyema
katika mashindano ya ligi kuu na pia
kuanzisha msingi mzuri wa timu za watoto.
“Dk Sulaiman ni Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa kampuni ya Al Fahim Group na vile vile
“Dk Sulaiman ni Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa kampuni ya Al Fahim Group na vile vile
alikuwa mkurugenzi wa kituo cha Royal Football Fund
(RFF) mbali ya kuwa
mchezaji wa mchezo wa chesi, ameahidi kusaidia
wachezaji chipukizi ili
kuwawezesha kushiriki katika mpira wa kulipwa,
tunaamini tutafika,” alisema.
No comments:
Post a Comment